Monday, January 21

Supu ya ng'ombe

   Kuna msemo wa kiswahili wasema, "Mgeni njoo, mwenyeji apone". Nimepata kuutumia vyema msemo huo kwa matendo muda huu ambapo wifi yangu amejifungua mtoto wa kike, hongera zake nyingi tu, toka kwa wana Menu Time. Sasa kwa mila zetu yapaswa aje kwa mama mkwe kulelewa kwa muda flani. Tukiongea kulelewa inahusisha suala la menu pia, na hapo ndo mwenyeji mie napoponea.
   Mama aliyejifungua anahitaji kula vyakula vyenye virutubisho vyote vinavyohitajika kutengeneza maziwa ya mtoto, maana ndo menu ya mtoto katika ile miezi ya kwanza mitatu na kuendelea. Hivyo suala zima la supu, uji, maji ya matunda, mtori na zaga zaga nyingine ziinahusika.
   Kupika nimefundishwa na mama mzazi, hivyo muda huu wa yeye mama kumpikia mkwe wake yaani mke wa mwanae wa kiume, mie ndo nazidi kuongeza ufundi zaidi wa mapishi kwa kujifunza toka kwake na pia kula vitamu.
   Moja ya mlo ambao lazima mama mtoto ale kila siku ni supu ya ng'ombe. Ntaja wafunza vyema namna ya kuipika ile inayotakiwa kwa mama aliyejifungua, pia ukienda kununua basi ununue upande upi ili upate ile supu inayohitajika, maana sio waenda nunua nyama tu kwasababu unanunua.

   Kwa karibu yaonekana hivi, na vipande vya nyma kidogo

  Iwapo unajua vyakula ambavyo mama aliyejifungua anapaswa kula, basi share nasi kupitia email address zetu.
   

No comments:

Post a Comment