Tuesday, December 4

Vyakula bora kwa aishie na VVU

  Tunasonga mbele na kukueleza vile vyakula mbavyo Rafiq aishie na Virusi vya Ukimwi, hupaswa kuvila ili kujenga afya yake, kujiimarisha na kuwa katika hali bora zaidi. Iwe umeanza kutumia dawa za kuongeza siku za kuishi yaani ARVs au haujaanza, vyakula hivi ni muhimu sana kwa yeyote aishie na VVU.
   Iwapo haugusi na hili, ila una Rafiq au mwanafamilia mwenye kuishi na VVU, basi si mbaya kushare nae hili jambo, ili naye awe katika hali nzuri ya kujihudumia katika mlo wake atakaokua anatengeneza.
   Leo tunaangalia vyakula vya asili na wanyama.
Hapa kuna:
    Kunde, Njegere, Maharagwe,  Njugumawe,  Fiwi, Soya, Karanga, Dengu, Choroko........

 
 
Nyama, Mayai, Maziwa, Dagaa, Samaki, Jibini, Senene na Kumbikumbi



 
Leo tumeangalia vyakula vya asili na wanyama. Kama tulivyosema mwanzo ...... ni juu yako   wewe kuangalia, je, ni urahisi upi kutokana na umbali, bei na upatikanaji wa vyakula hivyo, ndo vitakupelekea kuchagua na kuweza kuvitumia wewe, au kumtayarishia yule mwenye kuishi na VVU.
Iwapo una maoni, tafadhali yaandike sehemu ya maoni, na iwapo  una zaidi ya hapo, karibu kutuandikia kupitia info@menutimetz.com nasi tutakutejea au kushare na wengine.

No comments:

Post a Comment