Wednesday, December 12

Mapishi ya Rosti ya Ng'ombe na chapati

   Leo tunaangalia namna ya kupika rosti ya ng'ombe na chapati. Tutarejea kuwajuza namna ya kupika chapati na mahitaji ya utengenezaji wa chapati. Leo tuangalie hii rosti ya ng'ombe inapikwaje....

 Mahitaji:
  • Nyama ya ng'ombe kilo moja (yaweza kuwa ya mfupa au steki)
  • Chumvi kiasi
  • Kitunguu maji 1
  • Nyanya 2
  • Viazi ulaya 2
  • Pilipili hoho 1
  • Karoti 1
  • Pilipili manga kiasi
  • Kitunguu swaumu kiasi
  • Tangawizi kiasi
  • Mafuta kiasi
Hatua:
  • Chemsha nyama yako ikiwa umeikata vipande vipande, ongeza chumvi, kitunguu swaumu, tangawizi na pilipili manga. Ongeza maji kila inapokaukiwa na maji.
  • Baada ya nyama kuchemka vyema, weka sufuria safi motoni, ongeza mafuta kiasi, yakishapata moto ongeza chumvi kiasi, kisha weka vitunguu maji acha mpaka viive. Ongeza vitunguu swaumu, tangawizi kiasi koroga mpaka viive. Ongeza pilipili hoho, karoti na vipande vya viazi ulaya, koroga na acha viive vyema.
  • Ongeza nyama iliyochemka, acha viive vyema, kila inapokaukia ongeza supu iliyobaki kwenye nyama uliyochemsha. Baada ya kuchanganyika vyema, weka vipande vya nyanya na acha rosti ijitengeneze.
  • Ongeza Royco au Onga kama unapenda, kisha malizia na tui la kwanza la nazi, ambapo utakoroga rosti yako kuhakikisha haikatiki inapochemka.
  • Epua rosti yako tayari kwa kuliwa.
Picha ya rosti yetu ilitokea hivi. Na sisi tuliamua kuisindikiza na chapati.

      Jaribu pishi hili, kisha tujuze je, imetokeaje?? tutumie picha tushare na Rafiqs. Karibuni tuendelee kujifunza mapishi mbalimbali.

No comments:

Post a Comment