Monday, November 5

Samsung week - Golden Tulip Hotel

 Naendelea kukujuza yaliyojiri katika usiku huo wa sherehe ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na Samsung - Tanzania.
 Baada ya bites tulizokaribishwa ambazo zilikua sambamba na vinywaji, tulikaribishwa ndani, kuweza kuanza shughuli tuliyoitiwa pale Golden TulipHotel .

 
  Na muda wa msosi ulipofika, Menu Time ndipo tulipohusika zaidi. Kulikuwa na aina mbalimbali za vyakula, kuanzia salad, supu, nyama choma mpaka wali mweupe.
 
  Bakuli zasubiria kuweka supu tayari kwa wageni kuenjoy
 
Kulikua na supu aina mbili, na hii ni ya mboga mboga a.k.a veggie soup
 
Halafu kulikua na nyama ya ng'ombe ya kukaangwa 

Wakanikumbusha T.bonas nlipoona jiko na uwepo wa kuku choma

Kulikua na kuku waliopikwa kwa mchuzi .a.k.a chicken curry
 
Halafu kulikua na nyama ya ng'ombe iliyoungwa na mchicha na tui la nazi

Kulikua na nyama ya kondoo, ambayo nayo ilipikwa huku ikiwa na rojo

Nyama iliyokaangwa nayo ilikuwepo tayari kabisa kuliwa na wageni

Kulikua na kisamvu kilichoungwa na tui la nazi

Viazi vya kukaangwa navyo vilikuwepo, lakini sio katika mtindo wa chipsi
 
Shughuli haikamiliki bila ya mchele kuwepo, wali mweupe ulikuwepo pia

Halafu kukawa na wali wenye mbogamboga a.k.a veggie rice
 
Vikoromwezo lazima viwepo ili kukamilisha utamu wa menyu nzima
 
Halafu kulikuwepo na Salad za aina kadhaa... na hapa ndipo MT walipochanganyikiwa zaidi. Tuangalie aina ya salad walizokuwa nazo siku hiyo
Kwanza kulikua na green salad
 
Ya pili ilikua ni ya nyanya, machungwa, ndimu kwa mbali n.k

Salad ya veggies na mayai ya kuchemshwa nayo ilikuwepo

Kukawa na ile ya viazi vilivyochanganywa na mayonnaise, pembeni imerembwa na vipande vya matikiti maji
 
   Kiukweli meza ilipendeza mno, kutoka upangaji hadi ladha ya vyakula vilivyokua vimeandaliwa kusindikiza hiyo siku ya Samsung pale hoteli ya Golden Tulip iliyopo Masaki.

No comments:

Post a Comment