Thursday, July 26

Mikate Mikate Mikate

   Mara nyingi tumezoea kula mkate uliopikwa kwa kutumia unga wa ngano. Nimeamini binadamu ni watundu mno, au niseme wabunifu???..... naamini neno wabunifu litafaa zaidi. Wahenga walisema "tembea uone"... na sie leo tumejionea.
  Kutoka kwa Rafiqs zetu, Menu Time tumejuzwa maeneo ya kupata aina tofauti ya upikwaji wa mikate, nasi tukaona ni vyema kuwajuza. Najua wengi mtasema mbona mpiko huu wa mkate tunaujua..... si ndio? sawaaa wa kwanza ntakubali ila huu mwingine naamini ndo sie tutakua tunawajuza wengi wenu.
 Tunaongelea mkate wa kumimina, kama uonekanavyo kwenye picha hapo chini... huu unapatikana mitaa ya upanga uhindini kama wanavyopaita wenyewe.
                           

   Huu wa pili ni mkate wa tambi, yaani umetengenezwa kwa tambi. Sasa ni namna gani umetengenezwa bado hatujapata ubunifu wake, ila hivi karibuni vyote vikienda sawa tutawajuza, laaa tutawajulisha wapi unapatikana nawe uweze kuuonja.
 

    Mikate hii hupatikana kwa kutoa oda, yaani upige simu siku moja kabla ili waweze kukutengenezea maarn utamu wake ni kwamba uliwe siku hiyo hiyo au walau keshoye asubuhi yaani uchukuliwe jioni uliwe asubuhi lakini usiuweke ukae saaana, unakua kama umepoa hivi. 
                           
Shukrani za dhati ziwafikie Janeth, Peter na da Bridget kwa kutuonesha na kutuelekeza wapi twaweza kupata utamu huu.
  Kutoka pande za upanga, MenuTime yawajuza.

No comments:

Post a Comment