Thursday, July 26

Mokka City Cafe & Lounge ya City center mjini Dar iliyo salama

   Mjini Dar iliyo salama, naongelea katikati ya mjini haswaa, yaani pale Samora ambapo mambo yote unayapata kuanzia fundi wa saa, hadi wa simu. Yaani wenye mji wenyewe wanasema kila kitu hupatikana hata mihuri ya naniihii (jina limenitoka kidogo) inapatikana hapo, ndipo huu mgahawa ulipo. Unaitwa Mokka City Cafe & Lounge na hauna muda mrefu saana toka umefunguliwa, naongelea sio zaidi ya miezi mitatu hivi.
   Humo ndani kuna mengi muno muno, ila leo ngoja tuongelee machache ili nawe upate hamu ya kwenda kupatembelea hivi karibuni.
   Menu Time tutaongelea vimiminika tu siku ya leo... na tunaanza na hiki.
Tuliambiwa kinaitwa Ice Mocha na hivyo vipande unaona ni vya barafu. Sasa kinatengenezwaje ni siri yao ila MT tunadhibitisha utamu wake kwani baadhi ya wanachama wa MT walipata kukionja.
 
 
   Mara ya kwanza sisi kufika hapa tulilakiwa na harufu nzuri ya kahawa, yaani ukiingia tu ndani ya mlango unaachia tabasamu uwe mpenzi au sio mpenzi wa kahawa, ila harufu yake laaaaah, lazima uagizie kinywaji chochote kilichotengenezwa na kahawa.
Ya pili wanaiita Cappuccino

   Kila mmoja wetu ana mbwembwe zake katika idara yake. Kinyozi ajua kunyoa vyema na kuchonga style, msusi atakusuka nywele utadhani mkeka, basi na watengenezaji kahawa wa Mokka city nao wana mbwembwe zao katika kurembesha hiyo Cappuccino yao.
  Moja ya mbwembwe zao ni hii ambayo imerembwa mfano wa jani hapo juu.... nimependa ujuzi huu
 
   Wakati tunaendelea kushangaa urembo na mandhari, manager wa Mokka City aitwa  Ben akasema hiyo mbona cha mtoto,  kisha akatuletea Cappuccino ingine yenye urembo mfano wa nyumba ya buibui.
   Tazama usanii, ubunifu na kazi iliyofanyika hapo.

      Ukiwa mjini na unahitaji sehemu ya kupumzika , kupata kikombe cha kahawa, chai, iwe juisi, maji baridi hata soda, chakula na vinginevyo usisite kufika Mokka City Cafe & Lounge ambayo ipo barabara ya Samora, mkabala na jengo la IPS.
    Kutoka Mokka City Cafe & Lounge, LJM wa Menu Time nawapasha.

No comments:

Post a Comment