Thursday, May 19

Menyu ya Kitaani

Kinondoni, kona ya Best bite pale, nenda mbele kona ya kwanza kulia achana nayo, nenda mbele kona ya pili ingia, nenda mbele utakutana na gereji ya mabenz, wasalimie ndugu zetu kisha endelea mbele kidogo upande wa kulia utakuta kuna baa nzuri tu.
Sifa kubwa kuna bwawa la maji pale kwahiyo mbu ndo nyumbani kwao, lakini sio neno wanapigwa dawa mara kwa mara.
Hii sehemu inasifika sana kwa kupika nyama ya maana, namaanisha kuchoma nyama ya maana ya Ng'ombe na mwenzie Mbuzi. Sijajua wanaweka nini wakati wa kumarinate ila ni laini yaani kama inateleza flani mdomoni halafu ni tamu mno.
Hili ni moja ya jiko lao, nadhani wanayo kama matatu au manne.
 
 
Sasa hii ni mbuzi ya Tsh 8,000/= kaka alikua ananikatia, mie mwenzenu mgonjwa wa nyama choma yeuwiiiiiii
 
Halafu pembeni kuna chipsi zimekaushwa uzuri mno......


Baada ya ile nyama kukatwa na mchuzi wake huwa inaonekana hiviiiii, kama wataka kufungiwa ukalie kwingine, na sio pale pale.

Kama upo Dar Es Salaama na hujawahi patembelea hapa, nakusihi uende. Kama upo mkoa au nchi nyingine, siku ukija Dar fanya juu chini usiache pitia hapa upate utamu, au tuma rafiki kama utakua busy sana.
Nakutakia mchana mwema na Siku njema!!!!


No comments:

Post a Comment