Wednesday, May 11

Mapishi ya wali wa nazi, viazi na samaki kaanga

   Leo tunapika wali wa nazi, viazi vya kukaanga, mchemsho wa mboga za majani na samaki za kukaanga.

Mahitaji:
  • Mchele
  • Tui la nazi
  • Chumvi
  • Viazi
  • Kitunguu maji
  • Zucchin
  • karoti
  • French beans
  • Samaki
  • Tangawizi
  • Vinegar
  • Ndimu
  • Pilipili manga
  • Mafuta ya kupikia.
Hatua za kupika:
Tuanze na wali wa nazi
  • Tayarisha maji yenye tui la nazi na chumvi kidogo na uweke kwenye moto
  • Osha mchele tayari kwa kupikwa
  • Kabla maji hayajachemka, na yakiwa yamepata moto sana, ingiza mchele uliyo oshwa ndani ya sufuria
  • Pika wali katika moto mdogo hadi uive

  • Epua wali wako tayari kwa kuliwa.
Tuje kwenye viazi vya kukaanga
  • Menya maganda ya viazi
  • Osha viazi tayari kwa kupikwa
  • Weka viazi ndani ya sufuria yenye maji, chumvi kidogo na vitunguu tayari kwa kuchemshwa
  • Chemsha viazi kiasi
  • Epua viazi vyako na chuja maji uliyochemshia


  • Chukua kikaangio na weka mafuta ya kupikia
  • Kaanga viazi vyako mpaka vibadilike rangi ya brown na kuiva vyema
  • Epua viazi vvyako tayari kwa kuliwa.
Tupike mboga zetu
  • Chukua zucchini, karoti, french beans na giligilani


  • Katakata vipande vilivyo sawa
  • Viweke ndani ya sufuria na maji kiasi na chumvi kiasi


  • Chemsha kiasi na hakikisha visiive sana.
Tumalizie na Samaki za kukaanga
  • Safisha samaki vyema
  • Katakata vitunguu swaumu na tangawizi na kisha viponde
  • Katakata samaki kisha vichane kidogo kidogona kisu kuruhusu mchanganyiko uingie ndani ya samaki
  • Changanya Vitunguu swaumu na tangawizi vilivyopondwa na ndimu, mafuta ya kupika, vinegar pamoja na vipande vya samaki

  • Acha mchanganyiko huo uingie ndani ya vipande vya samaki kwa muda wa dk 30 - 45
  • Weka mafuta ya kupikia ndani ya kikaango na yaache yapate moto wa kutosha
  • Ingiza vipande vya samaki ndani ya mafuta na kaanga mpaka vipate rangi ya brown na viive kabisa
  • Epua samaki wako tayari kwa kuliwa.
Naamini, umejifunza vyema..... waweza kutuma mapishi yako kupitia menutimes@gmail.com
au kama una picha ya chakula ungependa iwekwe basi tuma kupitia anuani hiyo.
Karibuni.

No comments:

Post a Comment