Sunday, May 31

Yalojiri Nyama Choma Festival

     Jumamosi kumekua na matamasha kadhaa likiwemo Nyama Choma Festival, ambalo hili lilifanyika viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni.
   Kama ilivyoada ni tamasha linalokutanisha wachoma nyama mahiri kutoka sehemu mbalimbali kuja kuchoma nyama ili wahudhuriaji wapate kuonja na kufurahia nyama zenye ladha tofauti tofauti 
  Baadhi ya mambo tuliyoweza kuyanasa ni pamoja na nyama zilizokua zikiendelea kuchomwa katika mabanda mbalimbali

  Moshi kutoka kwenye majiko, huku baadhi ya nyama ipo tayari kwa kuuzwa

   Wateja na wauzaji busy katika kubadilishana biashara

   Majiko ya aina tofauti katika kuhakikisha ladha kamili yapatikanika yalikuwepo

   Matayarisho zaidi, huku nyama zikiendelea kuiva jikoni

 Kwa ukaribu zaidi

  Upande wa kati ulitengwa kwa wahudhuriaji kupata sehemu ya kukaa tena chini ya kivuli wakifurahia nyama pamoja na vinywaji

   Muziki pia ulikuwepo ikiwa ni mojawapo ya viburudisho wateja walipata

    Eneo moja llikua na utofauti wa uchomaji nyama wake, yaani wao hawakutumia majiko ya kawaida kama wengine bali walichimba shimo kiasi na kuweka mkaa kisha wakazungusha vipande vya nyama vilivyochomekwa kwenye vijiti vilivyochimbiwa ndani ya ardhi kuuzunguka moto uliokua unaziivisha taratibu. Hapa Mama Menutime akipata maelezo

  Na huo ndio muonekano wa nyama zilizowekwa tayari kwa kuivishwa na makaa yanayowaka yaliyopo katikati ya mzunguko wa vipande vya nyama

  Kwa ukaribu zaidi, umahiri na ubunifu wa uchomaji wa nyama. tulipata kuambiwa kijiti chenye mguu mmoja kilikua kinauzwa shilingi elfu arubaini za kitanzania. 

  Katika kupata habari zaidi, kwenye picha hapo juu, hao ni jumla ya mbuzi kumi waliowekwa. Na kutaka kujua je utumbo na mengineyo yanakwenda wapi.... angalia picha ifuatayo

   Supu ilikua inachemka ambapo ndani yake kuna utumbo wa mbuzi wale wanaochomwa. Hivyo basi kwa mahitaji ya supu ya utumbo wa mbuzi siku hii yalipatikanika kwa hawa kina kaka wenye style ya pekee ya uchomaji wa nyama.

     Kutoka Leaders ground, ambapo NCF ilikuwepo Jumamosi ya jana, hatuna la ziada wikiendi hii. Tunawatakia wiki njema na yenye mafanikio.

No comments:

Post a Comment