Saturday, May 30

Yalojiri Goat Race event

     Siku ya Jumamosi nzuri tu ambapo shughuli ya Goat race yaani mbio za mbuzi imefanyika katika viwanja vilivyopo Masaki na kuhudhuriwa na watu wengi kutoka sehemu mbalimbali Dar es salaam
    Theme ya mwaka huu ni India wear yaani mavazi ya kiasili ya wahindi. Hivyo wengi waliohudhuria walikua katika muonekano wa kiasia/ kihindi kama ilivyotakikanika na theme ya shughuli yenyewe. 
    Vyakula na vinywaji mbali mbali viliuzwa, huku michezo ya watoto ikiwepo kuwaburudisha watoto waliohudhuria.
    Tupate ushuhuda ya yalojiri katika Goat race ya 2015

Hakika walipendeza na muonekano huu

Mbuzi wakielekea kwenye uwanja wa mashindano

Kiongozi wa msafara wa mbuzi wanaoshindana

Mbuzi wamewekwa chini tayari kwa kushindana

Na mbio za mbuzi zilianza ambapo alishinda mbuzi nambari 6

Madafu, matunda yasiyo na msimu nayo yalikuwepo kupooza koo za waliohudhuria shughuli hii

Buffet kutoka Thai Kani ilikuwepo 
Pizza kutoka Bella Napoli ndio iliyoliwa na timu ya Menu Time iliyokuwepo uwanjani

 Zaidi ya hayo, kulikua na dansi za aina mbali mbali zikiwemo ngoma za kienyeji. Hatuna la ziadi kutoka viwanja vya Masaki ilipofanyika event ya Goat race 2015, 
  Tunaelekea Leaders Ground inapofanyika Nyama Choma Festival na tutarejea kuwajuza yanayojiri

No comments:

Post a Comment