Monday, August 25

Twaelekea nyumbani Moshi

   Tumefika salama salimini nyumbani, naongelea Moshi, Kilimanjaro. Mkoa upendwao mno na maarufu kwa kuwa napesa maana kina Mangi wanajua kuzitafuta na kuzitumia.
  Tutakua tunajuzana mengi yatakayojiri katika safari hii toka mwanzo hadi mwisho wake tukiwa pamoja hapa bloguni au kupitia social media accounts zetu.
  Tukipofika kama ilivyo ada lazima kutia sahihi pub ya nyumbani na hivyo tulilazimika kupita Meku's Bistro kuweka sahihi kabla ya yote.
  Sahihi ya leo ilikua hiviii, samaki rosti na vikorombwezo kadhaaa akisindikizwa na viepe

   Na mwingine alisindikizwa na wali mweupe

  Ukifika round about pale huna haja ya kuuliza sana, panajionesha. Tulichopenda zaidi ni huduma nzuri hasa toka kwa bi Maria na bwana Maulo ambaye ni mpishi.
Tutarejea tena na tena na tutaendelea kuwajuza yanayojiri pande za Moshi.

No comments:

Post a Comment