Tuesday, August 5

Mwanza, Mwanza a.k.a Rock city

   Jana asubuhi tuliamkia uwanja wa ndege tukiwa safarini kuja huku kuliko na ziwa Victoria. Tunaongelea Mwanza a..k.a Rock city ambapo wale samaki watamu hupatikanika.
  Mchana wa jana tukapita Villa Park kama ilivyo ada ukifika Mwanza shurti upate kukarinishwa, na mchana walitukaribisha kwa namna hii
   Kulikua na samaki aliyekaangwa kwa mafuta tu na chumvi bila ya kiungo kingine chochote

 Visindikizio vilikua, pilipili, kachumbari, mchuzi pamoja na ugali kama vionekanavyo kwa picha hapo chini

Halafu kulikua na samaki aliyepikwa kwa viungo almaarufu kwa jina la Brenda Fasi, kama aonekanavyo hapo chini. Huyu kapikwa na viungo vingi vikiwemo karoti, pilipil hoho, ndimu, pilipili kichaa, vitunguu na kadhalika ilimradi kumnogesha na alinoga kweli kweli

   Tupo kwa muda pande za Rock city na tunaamini, tutaendeleza kuwajuza vyema yote yanayojiri pande hii. Msimu wa Serengeti Fiesta umeanza...... Ni Shiida!

No comments:

Post a Comment