Thursday, July 10

Wikiendi ndefu na menu zake

  bado twaendelea kukujuza yalojiri katika hii long wikiendi ambapo ilianza Ijumaa hadi Jumatatu ambapo tulikua tunatimilisha sikukuu ya wakulima hapa tanzania.
  sasa siku ya Jumapili, tulipata kwenda kuosha macho viwanja vya sabasaba nikiwa na mama yangu, na baada yakutoka hapo na kufaidi mengi, tukaona tupite mgahawa mmoja katikati ya mji ujulikanao kama Mokka City lounge na menu tuliyoipata ni hii hapa chini...... karibuni
  Mimi kama kawaida yangu nilipata menu hii ambapo ipo hivi, ni vimikate vya pizza ambavyo ndani kuna vipande vya nyama ya kuku na viungo vingine, huku ikisindikizwa na salad pamoja na mayonnaise

Mama yeye alipata kujaribisha biriani ya kuku, na moja ya neno alitoa ni kwamba biriani hii ilikosa lile rojo la kibiriani ambalo walipata kitaani au mtu akilipika home, Uzuri mwisho wa siku alipata kuenjoy jinsi ilivyo maana upishi watofautiana, na ilikua ni vyema kujaribu mapishi mengine.

   Fanya kuwapitia hawa Mokka City lounge waliopo mjini katikati iwapo mida ya menu itakupata eneo hilo, au iwapo wataka kujaribisha mapishi ya aina tofauti.
   kutoka kwetu, kutoka wikiendi ndefu ndo tunakomea hapa na tutarejea kesho tuanze kuangalia wikiendi hii twaanzia wapi. Karibu kutujuza wapi mtakuwepo wewe na marafiki zako kupitia anwani yetu menutimes@gmail.com

No comments:

Post a Comment