Wednesday, September 11

Dar es salaam Food Fair Event ilivyokuwa....

   Nelwa Gelato walikuwepo pande za Botanical garden wakionesha ufundi wao wa utengenezaji wa ice cream.
   Hebu angalia ladha kadha wa kadha ambazo wanatengeneza

  Kuna ladha za strawberry, vanilla, chocolate na nyinginezo nyingi, ambapo tulipozijaribu kwa kweli utamu wake hauelezeki. Wapo sehemu kadhaa wakiuza bidhaa zao za ice cream

   Kutoka Arusha, tulikutana na Rafiqs ambao wao wana bidhaa tofauti tofauti, yaani wanatengeneza asali, kahawa na pia wanafanya ukarabati wa mashine za kutengenezea kahawa.
  Cha kwanza tunaangalia ni asali wanazotengeneza wenyewe na kuziuza kwa jumla ya fedha taslimu za kitanzania shilingi elfu kumi tu. 

   Kahawa zao hupakiwa katika mtindo huu, hivyo ukiona packaging hii jua una bidhaa ya ukwe'ee

   Wanaitwa EDELWEISS Coffee Estate, Arusha wanapatikana Njiro

   AK's cafe nao hawakubaki nyuma, walionesha msosi wa kwanza ni pasta yaani tambi

 Pia walikua na veggie rolls ambazo sauce waliyotumia hakika iliongeza utamu wa pekee, kwa namna ya kipekee

Walionesha ujuzi wao kwenye upande wa vimiminika pia

  Na burger zao walionesha nembo ya eneo lao la kazi, kwa kuweka vipeperushi vyenye jina lao

  Upande wa mwisho walikuwepo Rafiqs ambao hatutawaongelea sana angalia mwenyewe sanaa ya urembo na mapambo

Yummyy

  Pembeni kulikuwa na viunganishi hivi.....

  Hakika kila mpishi ana namna yake ya kuonesha kivutio cha menu yake kwa walaji wake

  Kihalali tulienjoy sana kuwepo pale na kuweza kuchukua machache ambayo tumeweza waonesha hapa. Tunaamini mmepata vyema kujua yalojiri.
  Kesho tutaona yaliyojiri kwenye Nyama choma festival ambayo tulihudhuria na kushiriki baada ya kutoka hapa.

No comments:

Post a Comment