Wednesday, August 7

Twaimalizia Iftar ya Airtel kwa wafanyakazi wake

  Sasa tumalizie yalojiri pale ambapo Airtel walifuturisha wafanyakazi wake mikoa mbalimbali, ila sisi twaripoti kutoka hapa hapa Dar iliyo salama. Karibu tumalizie...
Kwanza zilikuwepo tambi za usukari

Halafu kulikua na hili rojo, hatukudadisi sana lina nini ndani yake, maana muda haukuruhusu, tulikua busy kufuturu... upo?

   Kulikua na viazi ulaya vilivyopikwa na mchuzi, kwa rangi waonekana mtamu kwa ladha ni zaidi ya utamu

  Njugu mawe zenye sukari nazo zilikuwepo, zilizoungwa vyema na tui la nazi

Mihogo ndio msimu wake haswaa, nayo ilikuwepo iliyopikwa na tui la nazi na iliki kama ilivyo ada

  Halafu pale ambapo wengi hupapenda kwenye ndizi mzuzu zilizopikwa kwa tui la nazi na iliki zikapikika na kukolea ladha

  Uone tu mpangilio wa mezani ulivyotulia tayari kwa waalikwa kujinafasi

Kwa upande mwingine wa meza ulivyokaa, ili uone mambo mengi kwa pamoja


  Kutoka Airtel house iliyopo moroco, Kinondoni, Dar iliyo salama, Tanzania hatuna la ziada zaidi ya kuwatakia siku njema na mfungo mwema wa siku chache zilizobaki za mwezi mtukufu wa Ramadhan.


No comments:

Post a Comment