Wednesday, July 31

Twaendelea na Iftar ya Airtel

   ..... Tunaendelea kuwaonesha yalojiri katika Iftar iliyoandaliwa na Kampuni ya simu ya Airtel pale Serena.
    Mpangilio wa kukaa ulikua hivi...

  Kwa ukaribu zaidi, paliandaliwa very simple and classic

 Sasa ndo tukaanza yale mambo yetu yaliyotupeleka pale, hapo kuna wali wenye viungo ambao unajulikana kama wali mchafu

Halafu kuna wali mweupe ulopikwa kwa tui la nazi

  Sambusa za nyama nazo zilikuwemo, za motooooo!!

  Halafu kulikua na hivi, jina lake hatukulipata (msaada tutani Rafiqs kutujuza jina) ila ndani zilikua na mbogamboga

Chapati za kusukuma zilikuwepo, ukiziona wajua za kusukuma ila ukizila kama za maji kwa ulaini wake. Hakika msukumaji ana mkono mzuri

  Viazi ulaya vilivyokaangwa na viungo navyo vilikuwepo, juu yake vilimwagiwa vitunguu na majani yale maalumu kwa kuongeza utamu na ladha 

   Kama ilivyo ada, kwenye msosi wowote unaoandaliwa, kuku a.k.a vyuku a.k.a kwiyoooz lazima wawepo, basi hawa walitengenezwa kwa namna ya utofauti kidogo, ila mwisho wa siku utamu ulikuwepo

  Waweza jiuliza hii ilikua futari au mengineyo? Ni hivi mualiko wa futari unapotolewa, waalikwa huwa wanatoka dini tofauti wakiwemo wasio funga siku hiyo, hivyo basi inapaswa kuwafikiria wao pia na kuwatayarishia msosi ambao wataweza ula na kufurahia pamoja na wengine.
   Tutarejea kesho kuendelea na picha, maana mambo yalikua mengi atiiii!!

No comments:

Post a Comment