Monday, June 25

Wali Mweupe.

Wali mweupe a.k.a majimaji waweza kuliwa na mboga za aina mbali mbali, hii itategemea na upatikanaji wa mboga, mahala ulipo au mapenzi yako wewe mlaji. MT imeonelea ni vema tukaona mboga zinazopendelewa na wakazi wengi wa Tanzania.

Wali nyama, ni moja ya menu inayopendwa na wakazi wengi wa Tanzania na inapatikana kwa urahisi pia.
 Wali wa samaki pia unapatikana na unapendwa sana, ukiingia hoteli yoyote Tanzania, wali samaki ni moja kati ya menu kuu.
 Ningeisahau wali kuku wadau wangenitoa macho, wali kwa kuku ni moja kati ya menu nzuri na tamu sana, awe kuku wa kukaanga ama wa mchuzi.
 Karibu Tanzania, Karibu Wali Mweupe lakini piaaaaa Karibu Menu Time.

No comments:

Post a Comment