Monday, May 2

Msaranga Special ya Golden shower - Moshi.

Mchana wa leo nimepelekwa na wenyeji wangu sehemu inaitwa Golden Shower. Niliambiwa kuna lunch special inatayarishwa yaitwa Msaranga Special. Binafsi niliagiza na viazi vya kuponda, Rogertus aliagiza na wali na Mkabita yeye aliagiza Fillet steak na chipsi.
Tulipofika wapishi ndo wakaingia kazini, nikapata bahati ya kufundishwa namna ya kupika hiyo Masaranga Special na Fillet steak. Naamini wali, viazi vya kuponda na chipsi tunajua kuvipika.
Naomba kushare na wewe mafundisho niliyoyapata..... Karibu.

Mahitaji:
  • Robo kilo ya fillet steak
  • Vitunguu swaumu (utavisaga)
  • Tangawizi (utaisaga)
  • Chumvi
  • Soya sauce
  • Vinegar
  • Kilo moja ya mdudu a.k.a pork (kata vipande vya wastan)
  • Pilipili hoho 1 (katakata vipande vidogo vidogo)
  • Royco curry powder
  • Nyanya 2 (zikwaruze / pondaponda)
  • Giligilani a.k.a korienda
Hatua za kupika:
Tuanze na fillet steak
  • Kwanza inapaswa kuimarinate nyama (kuiongeza ulaini na ladha), na hii inafanyika kwa kuchanganya vinegar, mafuta ya kupikia kidogo, soya sauce kidogo, tangawizi, kitunguu swaumu na chumvi kidogo kisha unaipaka nyama na kuiacha ikolee kwa muda 
  • Chukua kikaangio na uweke jikoni, ongeza mafuta ya kula na yapashe moto kwa muda
  • Kikaango na mafuta vikishapata moto, epua na uweke pembeni
  • Weka nyama iliyokua marinated kwenye kikaango, kisha kirejeshe kwenye moto
  •  
  • Wacha nyama iive kwa dk tano kisha igeuze iive upande wa pili kwa dakika 5 pia
  • Epua nyama yako tayari kwa kuliwa
Twende kwenye namna ya kupika hiyo Msaranga Special
  • Kwanza chemsha mdudu a.k.a pork pekee mpaka aive
  • Weka kikaango kwenye moto
  • Kisha ongeza mafuta, chumvi, vitunguu maji na pilipili hoho
  • Ongeza Royco mchuzi mix na koroga vichanganyike haswa
  •  
     
     
  • Ongeza nyanya ndani ya mchanganyiko huo ili upate ile rosti
  • Weka chumvi kiasi
  • Ongeza nyama ile tuliyochemsha, kisha weka soya souce kidogo
  • Ongeza maji uliyochemshia pork pale unapoona inakaukia
  •  
     
     
  • Weka giligilani a.k.a korienda
  • Tayari mlo upo tayari kwa kuliwa

  • Ukiweka mboga yako tayari na chakula cha kulia, ndo itatokea hivi:


Kama umependa mapishi, karibu upike na nitumie picha tuipate kushare na wenzetu
Asanteni Golden Shower

No comments:

Post a Comment