Tuesday, May 3

Wali na Machalari- Lunch ya leo

Mchana wa leo nilikua na hamu ya kula chakula cha nyumbani. Nkawaomba wenyeji wangu wanipeleke ntakapopata hicho chakula. Moshi mjini karibu na TRA na Tanesco kuna sehemu yaitwa "Kwa Sigi". Hapo unapata menyu kadhaa za ukweli. Kuanzia ugali, mlenda, machalari, wali, samaki watoto a.k.a dagaa wote unapata hapo. Ukitembelea Moshi usiache kupitia hapo aiseeee.



Niliagizia wali na ndizi nyama, ni tamuuuu muno muno. Nkashushia na glasi ya mtindi freshhhh toka kwa ng'ombe.

No comments:

Post a Comment