Sunday, May 1

Macaroni na Nyama ya kusaga

       Jumamosi ya tarehe 30.04.2011 Rafiqs zangu waliniambia wanapita kutoka ofisini wanaenda kwenye shughuli zao. Mida watakayopita ni ile mida ya Lunch, ikabidi nijipange. Nkaamua leo naingia jikoni mwenyewe. Tafutatafuta cha kupika, nkakutana na pakiti la macaroni kabatini na nyama ya kusaga kwa  jokofu. Nkakumbuka niliwahi fundishwa na mama yangu pishi hili. 
Karibu....Ukilipenda jaribu, halafu nitumie picha ya menu (chakula) itakavyotokea !!

Mahitaji:
  • Pakiti la macaroni  1            
  • Pilipili manga (utaisaga)
  • Chumvi
  • Blue band / Tanbond
  • Nyama ya kusaga
  • Kitunguu maji kikubwa 1 (kikate vipande vidogo vidogo)
  • Vitunguu swaumu (utaviponda)
  • Tangawizi (utaiponda)
  • Viazi ulaya (vikate vipande vidogo vidogo)
  • Biringanya (ikate vipande vidogo vidogo)
  • Pilipili hoho (ikate vipande vidogo vidogo)
  • Pilipili kali (iache nzima)
  • Karoti (ikate vipande vidogo vidogo)
  • Nyanya 2 (zikate vipande vidogo vidogo)
  • Tui la nazi (binafsi napenda lile la kukuna na kukamua mwenyewe)
  •               


Hatua za kupika:
Tuanze na Macaroni
  • Tayarisha sufuria safi, weka maji ya kutosha
  • Ongeza chumvi kiasi na pilipili manga iliyosagwa
  • Weka jikoni na yaache mpaka yachemke
  •                   
  • Ingiza macaroni kwenye maji yaliyochemka.
  • Japokua pakiti nyingi zinaandika kuwa muda wa kupika ni dakika 9 - 10, mi nashauri uhakikishe uivaji kwa kuzionja (unaweza kulisha watu kibichi)

  • Baada ya kuiva epua sufuria
  • Tayarisha chujio na mimina macaroni ndani ya chujio ili kuchuja maji uliyochemshia macaroni
  • Chukua maji yasiyo moto wala baridi miminia juu ya macaroni yakiwa bado ndani ya chujio
     
  • Rejesha sufuria uliyochemshia macaroni kwenye jiko huku ukiwa umepunguza sana moto
  • Weka Blueband/ Tanbond ndani ya sufuria yako na iacha iyeyuke vyema 
  • Rejesha macaroni ndani ya sufuria yenye Blueband/ Tanbond
  • Waweza ongeza pilipili manga iliyosagwa kama ukipenda
  • Koroga vyema kwa dakika 2 ili mchanganyiko wa macaroni, pilipili manga na Blueband/ Tanbond ukolee vyema 
  • Macaroni yako yapo tayari kwa kuchanganywa na mboga.
  • Epua sufuria weka pembeni na zima jiko


Tumalizie na Nyama ya kusaga:
  • Tayarisha sufuria safi, weka nyama ya kusaga peke yake bila ya kuweka maji
  • Ongeza chumvi kiasi, tangawizi na kitunguu swaumu
  • Weka sufuria lenye huo mchanganyiko kwenye jiko na washa jiko
  • Ongeza maji moto safi kila mara pale nyama inapokaukia
  • Funikia sufuria ili nyama ipate kuiva taratibu, hakikisha nyama imeiva vyema (ionje kama imeiva)
  • Baada ya kuiva epua nyama iweke kwenye chombo kingine pembeni.

  • Rudisha sufuria jikoni na weka mafuta ya kupikia kama vijiko vitatu
  • Ongeza chumvi kidogo, kisha weka vitunguu maji. koroga mchanganyiko huo (lazma utasikia harufu nzuri ya vitunguu vinaiva)
  • Vitunguu vikishaiva na kubadilika rangi ongeza pilipili kali moja bila kuikata
  • Ongeza vipande vya viazi na karoti na koroga
  • Ongeza biringanya, pilipili hoho na mchuzi ambao utakua upo katika ile nyama tuliyochemsha
  • Ongeza viungo kama vile vya pilau n.k (hapa inategemea unapenda viungo vipi, maana vipo vingi)

  • Vikishaiva ongeza nyanya, na ukorege kiasi kisha acha vichemke kidogo ili kutengeneza rojo
  • Weka nyama ya kusaga koroga vizuri huo mchanganyiko kisha acha kidogo vikolee
  • Waweza weka Royco mchuzi mix kama utapenda (mimi niliweka) kisha korogo rosti hilo
  • Malizia na tui na hakikisha unakoroga tui lisije kata
  • Baada ya tui kuiva vyema epua mboga yako tayari kwa kuchanganya na macaroni na kuliwa

  • Chukua chombo kingine tofauti, kikavu na kisafi (hotpot inafaa sana)
  • Weka macaroni yako kidogo, kisha unaweka mboga ya nyama ya kusaga kidogo kidogo huku unakoroga
  • Hakikisha macaroni na nyama vinachanganyika vyema.
  • Pakua chakula chako tayari kwa kuliwa.


Kama una swali, au maoni karibu sana sana!!!
Kama una mapishi yako unataka kutuletea karibu sana sana!!



3 comments: