Monday, May 23

Kitimoto ya Kinondoni

Katika pitapita yangu mitaa ya Kinondoni, kama unatokea Salenda baada ya makaburi kona ya kwanza kushoto kama unaenda Bar ya Bamboo, mbele ya gereji upande wa kushoto kuna contena mbili. Ukifika pale tafuta sehemu ya kuegesha gari kama una usafiri, halafu ingia hapo Ulizia ya Kuchoma.
Huyu jamaa sijui anaichomaje ila ikifika saa 12 na dakika kadhaa jioni, mzigo wote unakua umeisha. Sijajua kwa siku anauza kilo ngapi. Unaweza kuweka oda yako mapema kwa kumpigia simu namba 0754 228 502, halafu unaongea na Ellia unamwelezea mahitaji yako , baada ya muda unafika na kupata oda yako safi inakusubiri.
huu ni mfano tu wa ya kuchoma, ila kuna ya rosti na aina kadhaa za upishi.

Sijawahi kujua kwanini huwa chumvi inawekwa nyingi sana pale mteja anapoagiza chakula, ntatafuta sababu ni nini haswa halafu ntakuhadithia.


No comments:

Post a Comment