Thursday, September 5

Heshima Ya Chakula.

Chakula ni kiungo muhimu katika maisha ya kila siku ya mwanadamu, katika hali ya kawaida huwezi kupitisha siku bila kuwaza kuhusu nini utakula,
  Hapo kuna wali mchafu yaani pilau, kachumbari, nyama ya kuku na ng'ombe pamoja na ndizi

    Chakula kinaweza kutumika kama suluhisho kati ya watu ambao hawana maelewano mema, mfano kama kuna watu wamekwazana na unapenda kuona wanapatana na kurudi kuwa marafiki basi tumia chakula kuwaunganisha. Unaweza ukapika chakula kwako na kuwakaribisha wote wawili waje kula chakula pamoja ama waweza kwenda hotelini na mkashiriki nao mlo pamoja.
  Na mwaweza anza na matunda

 Ukiondoa kukutana nyumbani mwaweza toka mkaenda mgahawani na kuyamaliza


Chakula bado ni kiungo muhimu pia katika shughuli mbalimbali, Sherehe za Harusi, Kitchen Party, Sikukuu za kuzaliwa(Birthday).

Muonekano wa wapi menu inawekwa ni muhimu sana ili kuwapa hamu ya kula wale walaji wako

Halafu kuna zile menu tunazokula tukiwa tumeketi chini huku twashea sahani au sinia kwa pamoja.

Chakula kitakutumikia kadri unavokiagiza, kitakufurahisha kama utataka furaha na kitakukera kama hutokifurahia. Furahia mlo wako mara zote..

No comments:

Post a Comment