Friday, July 12

Nyama choma ya Kilema Moshi, Kilimanjaro

   Bado tuko pande za Kilimanjaro, Moshi, Marangu, Kilema ambako leo menu yao ya mchana ilikua ni nyama choma ya Mbuzi. Lakini kawaida yao wakikutana zaidi ya watatu tu, ni sababu tosha ya kuchinja mbuzi au ng'ombe tayari kwa starehe, huku tukishushia na mbege.
   Sasa hapo chini tayari Mbuzi keshatendewa haki

   Baada ya  muda kina baba, mangis wakawa na kazi ya kuchoma lakini kinyumbani zaidi, yaani ile ya kuwachomeka kwa vijiti afu unawasha moto na nyma inaiva taratibu.

   Ndo waishivyo Rafiqs zetu wa uchaggani, kina mangi na watoto zao. Kutoka Kilema, Moshi, asante sana Tonny kwa kutuwakilisha Menu Time.

No comments:

Post a Comment