Sunday, May 29

Nipo Kinondoni bado

Leo nilipigiwa simu na rafiq yangu Janeth ambaye alivutiwa na menyu ya tarehe 23, kitimoto ya Kinondoni. , baada ya kuona picha ya ile menyu alipatwa na hamu ya kwenda kuijaribu. Baada ya kumuelekeza vyema na kumpatia namba ya kaka alimpigia simu na kuweka oda ya kutosha jamii aliyokua nayo. Jumla walikua watu kama saba, na hizi ni picha alizonitumia.

Walimuomba mpishi awapikie Kitimoto ya aina yeyote itakayowafurahisha, na baada ya nusu saa, kaka alirejea na sahani mezani. Aliwapikia Makange ya Kitimoto.


Janeth anasema kuwa katika muda wa chini ya dakika kumi, kimya kilitanda mezani na hali ilibadilika na kilo 2 zilizowekwa mezani zilitoweka. Ghafla sahani ilibakia hivi:

Sahani ya pembeni kama vile chumvi na pilipili havijaguswa...... Ila inaonesha jinsi gani walifurahia chakula kilichotayarishwa kwa ajili yao.
Asante Janeth kwa habari na picha.

No comments:

Post a Comment