Tuesday, May 28

Cha mchana Jumanne hii ni .......

   Bado tuko pande zilezile za Samaki Samaki ya mjini posta. Dar iliyo salama ukisema mjini shurti utaje na posta kidogo ndo tuende sawa. Sasa basi kama ilivyo kwa wengi ukienda sehemu kula unakua na kampani aidha awe ndugu, rafiq, mfanyakazi mwenzio au hata adui yaani mnaenda kuzinguana sehemu ya kula ili kumalize tofauti zenu.
   Sahani ya kampani tuliyokua nayo ni hii hapa, yaani yeye alipenda zaidi mlo huu kama menu yake ya mchana hapa Samaki samaki

  Kama kawa viazi vyao vina saizi tofauti kidogo, ambapo Rafq aliagiza na ngisi a.k.a calamari

  Vikorombezo kwa pembeni, wakina pilipili, ndimu, mayonnaise na tomato sauce waliambatanishwa kuongeza ladha kwa Rafiq. Mboga za majani nazo pia huwekwa kwa mbali katika  mlo huu ili kuhakikisha unapata mlo proper

   Karibu kushare nasi menu uipatayo mida ya mchana ili nasi tushee na wao!! barua pepe ni ileile menutimes@gmail.com

No comments:

Post a Comment