Monday, May 27

Chakula cha mchana

   Wiki hii tutaongelea menu mbalimbali ambazo waweza kuzila/ kuzipata mida ya mchana, iwe upo mgahawani, hotelini, ofisini, nyumbani au penginepo ambapo msosi unapatikana.
    Waweza share nasi ni menu gani unapata nyakati za mchana na pia utueleze unaipatia wapi na hata inakucost pesa ngapi. 
 Tupo pande za Samaki Samaki iliyopo katikati ya jiji la Dar iliyo salama pale kwenye jengo jipya. karibu uwatembelee.


   Chipsi zao ni zile zipo katika style hiyo, aina ya mkato wa vipande vikubwa. Halafu pembeni ni vipande vya samaki vikisindikizwa na mchicha na vikorombwezo vya pilipili, mayonnaise, tomato sauce na ndimu.
      Ukifika ulizia Bruce lee fish. Naamini yapatikana katika maeneo yote ya Samaki samaki namaanisha mjini, survey na Mbezi.

No comments:

Post a Comment