Sunday, April 14

Ya mwisho kuhusu Toto day ya kwanza ya 23.03.2013

   Kitu kimoja tulishauriana na partner wetu bwana Mutta wa K.A.B.L.E Inc ni kwamba tuwe na kumbukumbu ya shughuli hii  zaidi ya picha. Na akaja na wazo la kutengeneza chaa za viganja vya mikono yetu ambapo watoto walilowanisha viganja vya mikono yao na kuweka stamp kwenye kitambaa cheupe ambacho kitatumika kama kumbukumbu ya siku hiyo.
   Rafiqs wakiwa tayari kuweka alama ya kiganja

Toto akisaidiwa na mamii kuweka alama ya kiganja

LJM wa Menu Time, akimsaidia mchina kuweka nembo kwenye kitambaa cha ukumbusho

Baada ya hapo, LJM akaweka alama ya kiganja kwenye kitambaa cha ukumbusho

Muonekano wa kitambaa cha ukumbushoulikua hivi
   Watayarishaji wa Toto day ni K.A.B.L.E na Menu Time wakiwawakilishwa na Mutta na LJM

   Tunashukuru Mungu vyote vilienda sawa, na mida ya jioni tulinyoosha mikono ya shukrani na pumzi ndefu. It was time to exhale!!!
  Kutoka Mbalamwezi Beach Club iliyopo Kawe, naripoti tukio la Toto Day, ni LJM wa Menu Time!! Asanteni kwa kuwa nasi na kutembelea www.menutime.blogspot.com

No comments:

Post a Comment