Saturday, April 13

Tunamalizia yaliyojiri 23.03.2013

   Tunamalizia kukujuza yale yaliyotokea siku ya Toto day, na labda tuseme mapema kuwa, kuna nyingine itakuja hapo mbeleni, kwani tumeona ni jambo zuri na shughuli nzuri ya watoto kukutana na pia shughuli hii ina nia nzuri na manufaa kwa watoto yatima.
   Tumalizie na picha zilizobaki zinazojieleza vyema
Kutoka Sayona tulikunywa juisi na soda za kutosha, na baada ya menu tulishushia na maji yao, Shukrani za dhati kwao Sayona kwa kutusababishia upande wa vimiminika

   Achick investment nae alifika on time na popcorn za ladha ya chumvi na caramel, yaani zilitafunwa kwa raha zetu na zilizobaki Malaika Orphanage Foundation kids walibeba maana ilikua ni siku yao, Asante sana Akuku wa Achick Investment

   Muda wa chakula ulipofika Mbalamwezi Beach Club ndio waliandaa mpango mzima na kwa wageni kama tulivyotangaza, sahani iliuzwa shilingi 10,000/- tu za kitanzania ambapo kulikua na wali wa veggies, chipsi kiasi, kipande cha kuku, sausage pamoja na salad, na unapata juisi au soda ya Sayona kwa gharama hiyo hiyo. Asanteni sana Mbalamwezi Beach Club.

   Tuliuza sahani za kutosha kwa Rafiqs waliokuja kutoa support siku hiyo, na kwa wote walioweza kuhudhuria tunawashukuru sana, na tukutane Toto day ingine inayokuja soon soon!!

   Kutoka Malaika Orphanage Foundation, watoto wakifurahia menu...... kabla hatujaendelea na michezo mingine mingi tu

   Dada Hakika akiwa busy kuwaserve watoto na kuhakikisha wote wamepata mlo wa mchana, Hawaa pia alisaidia zoezi hili na wengineo, Asanteni nyote

  Tulisema menu itakuwepo na tulikula vya kutosha. Tunaamini kwa umoja na ushirikiano tuliopata kutoka Sayona, Achick investment pamoja na Mbalamwezi Beach club, tuliweza kuhakikisha watoto wote wamepata kufurahi siku hiyo kadri ya uwezo wetu tulioweza. Iwapo kuna lolote lilienda kinyume na ilivyotegemewa, tunaomba radhi kwani sote ni binadamnu na tutayabadilisha kwa kuboresha zaidi!!

No comments:

Post a Comment