Friday, June 1

Senene

 Hawa ni viumbe maarufu  sana huko Mkoani Kagera na wanaheshimiwa sana, ni mlo wenye historia nzuri ya kimapenzi tuseme. Ni hivi ukiona mchumba wa kihaya kakuletea hawa viumbe kwenye kisosi basi ujue siku ya kurudisha hicho kisosi, shurti kuwepo na kitu au vitu vya gharama sana. Picha hii imetumwa na kaka yetu pia Rafiq yetu wa kutoka mikoa hiyo, ila kwa sasa anaishi Kigoma.

 Asante Victor mashobe a.k.a Baba Ruge"Ronny".
Endelea kututembelea, na kututumia picha za menu kadhaa kutoka Kagera hadi Kigoma. Karibu tena tena na tena.

No comments:

Post a Comment