Thursday, June 30

Menyu ya Asubuhi - Mlimani City

Rafiqs wengine wao hupenda kufungua vinywa vyao na chai ya rangi, kuna wa chai ya maziwa, kuna wale wa Kahawa yenye maziwa, Kahawa nyeusi na aina kadha wa kadha.Yawezekana ni mazoea, au ni hamu uliyoamka nayo, kwamba leo nataka ninywe chai yenye ndimu asubuhi hii au maziwa mgando ilimradi tu vile hamu inapokupeleka.
Rafiqs hawa walikua Mlimani City na waliamua kufungua vinywa vyao kwa Cappuccino, Kahawa nyeusi na vitafunwa. Aliyekua anakunywa Kahawa nyeusi hakuweka sukari ila kitafunwa chake kilikua na sukari mno, binafsi nikahisi basi vikichanganyika kinywani utamu unakua vile anavyotaka.
Kuna wale babu zetu na hata vijana wanakunywaga ile kahawa chunguuuu na kashata mtaani, nawaona kama wanakua wamejiwekea hesabu/ vipimo flani hivi mdomoni, yaani fundo hii na kiasi cha kipande hiki vinaenda kusawazishana mdomoni... Ubunifu katika mlo au???Karibu tuwaone wa Mlimani City...


Rafiq, Iwapo ungependa kutuonesha Kifungua kinywa chako, tuwasiliane kupitia menutimes@gmail.com

No comments:

Post a Comment