Thursday, June 30

Menyu ya Asubuhi - Mbagala

Katika pitapita yangu nilikutana na Rafiq anatengeneza vitafunwa vyaitwa Vitumbua. Tayari alikua ameshachanganya na nilimkuta katika steji za mwisho. Ilikua asubuhi kama saa 2, akanieleza kila siku huwa anavipikia hapo hapo na kuuzia hapo hapo. Pembeni kuna meza, viti na chupa ya chai unajisevia, unalipa kisha unasepa.
Vitumbua vina kikaangio chake maalum, na sio kwenye kikaangio cha kawaida. Ule muonekano wake watokana na shape ya kikaangio chake.

Kama nilivyosema nilimkuta tayari keshaanza mapishi, kuna nafasi sehemu moja tu ya kikaangio

Hapa anamimina mchanganyiko kwenye kikaango

Mafuta yanaongezwa kidogo, ili kitumbua kisije kukaukia kwenye kikaango

Kikishaiva upande mmoja, kinageuzwa upande wa pili kiweze kuiva vyema, kisha huepuliwa na kuwekwa kwenye sinia tayari kwa mauzo.

Na kwa shilingi 100/= tu za kitanzania unapata Kitumbua chako, ukishushia na chai , siku inaanza vyema. Vitumbua vyaweza kuliwa muda wowote sio lazma asubuhi tu. Wengine hupenda kuweka kuwa moja ya mlo wa sherehe.
Nilipokwazika mie, ni kutokuwa na kawa au mfuniko flani kuweza kuvitunza katika sehemu salama zaidi. Ila tulizungumza, alikubali kuandaa kijisanduku cha kuuzia vitumbua vyake.

Karibu kutoa maoni yako, tuma barua pepe kupitia menutimes@gmail.com

No comments:

Post a Comment