Wednesday, June 29

Menyu ya Asubuhi a.k.a Breakfast - Nyumbani

Toka nyumbani kuna siku ambazo binafsi nafungua kinywa na uji wa ulezi. Huu huwa unapikwa na mama mzazi. Yaliyomo humo ndani ni pamoja na Unga wenyewe wa ulezi, maziwa freshi, siagi, mtindi kiaina, basi unakuwa na ladha flani tamu, ngumu kuelezea kidogo.
Waweza upata huu unga wa Ulezi toka kwenye Supermarkets mbalimbali. Huu uji wa ulezi una mapishi tofautitofauti na unanyweka sehemu nyingi sana. Kuna kina mama wanaupika, wanaweka kwenye thermos a.k.a chupa za kuwekea chai/ maji moto, kisha huenda kuuza. unapendwa sana!

Kuna siku ntakujuza namna ya kuupika utokee na utamu naotaka kukueleza. Kwa leo furahia picha yake, Karibu!!


Kikombe kimoja tu chantosha kuanza siku vyema!

No comments:

Post a Comment