Monday, June 20

Menyu toka kwa Rafiq

Rafiq alipata mualiko pande za Kariakoo - Dar es salaam - Tanzania!!.
Na hii ndio picha ya menyu aliyoandaliwa na Rafiqs zake

Haswa paliponifikisha ni suala zima la ubunifu, kama huna zulia na muda wa menyu umefika, tandika magazeti ambayo ulishayasoma chini na andaa menyu yako, kisha waite rafiqs wakaribie. Mwisho wa siku kinachojalisha ni mwito na namna ya pekee uliyowakumbuka na kuwaandalia.
Menyu imekamilika: Msosi kamili, Tunda, Juisi, Chai, halafu Kachumbari nayoooooooo laaah!! hakika walifurahi!!

Asante sana Vincent Koola kwa kushare nasi picha hii nzuri.

Karibu kushare nasi picha za msosi: aidha umeupika, umepikiwa, umealikwa kula, umejialika au hata umeenda kununua.Piga picha na tutumie picha yako kwetu kupitia anwani yetu ambayo ni menutimes@gmail.com

No comments:

Post a Comment