Wednesday, May 1

Upishi wa viazi vyenye maganda

   Kuna namna tofauti ya kupika viazi yaani vile vya kukaanga. Hii ni pale unapoamua kupika pamoja na maganda yake.
   Cha kuzingatia ni kuhakikisha unaviosha vyema viazi vyako kabla ya kuvipika, hakikisha mchanga wote umetoka na viazi ni visafi mno.
    Kisha kata vipande vya ukubwa kiasi na viweke kwenye sufuria yenya maji safi. Katakata vitunguu, kisha ongeza chumvi na pilipili manga kidogo kisha weka kwenye jiko na viache vipate kuchemka kidogo sana, vilainike kwa mbali.
   Epua viazi vyako na uchuje maji, kisha weka kikaangio kwenye jiko, weka mafuta na yakipata moto, weka viazi viweze kukaangika vyema. (usimenye maganda).
    Viazi vikishaiva na kugeuka rangi, epua tayari kwa kuliwa, vipange kwenye chombo safi kama sinia kisha kwaruzia jibini kwa juu na karibisha rafiqs mlo wa usiku.
    Ndizi ni aina ya mzuzu ambapo unazimenya kisha wavikata katikati na kuvikaanga vyema mpaka ziive. Epua tayari kwa kuliwa.
    Waweza kula na mboga yeyote uipendayo!!!


No comments:

Post a Comment