Tuesday, May 21

Kifungua kinywa

   Leo tumekaa kimaswali maswali zaidi... 
  La kwanza, Jumanne ya leo umefungua kinywa wapi??? umekula ukiwa nyumbani? kitaani?eneo la kazi? mgahawani? njiani? bar?au wapi?
  Swali la pili ntakuuliza, ni je, umefungua kinywa aje??? tumekula kitumbua kama mimi? maandazi? mikate? mihogo? viazi vitamu? sandwich? supu? soseji? juisi? chapati? kiporo cha jana? au? mmmh tuambizane
  Swali la tatu je, ulikua unafungua kinywa na nani? familia? wafanyakazi wenzio? wafanyabiashara wenzio? wana wa kitaa? washkaji? Rafiqs? maadui katika kuleta amani? Mashostito? au peke yakooo?? tujuze!!


   Kifungua kiinywa changu asubuhi ya leo kilikua hivyo hapo juu. Chai ya rangi, vitumbua viwili na soseji moja, niliipata nikiwa eneo la kazi, pamoja na Rafiqs na wafanyakazi wenzangu.
   Anwani ni menutimes@gmail.com ndo tunapopatikana.

No comments:

Post a Comment