Tuesday, April 16

Menyu a.k.a Menu za Kibo Business a.k.a Mbuzini

   Mitaa ya Kinondoni hapa Dar iliyo salama ndipo wanapopatikana hawa mashujaa wa kupika foil. Naongelea foil ya mbuzi na ya ng'ombe ambapo unaikuta tayari ishawiva, wanakuja nayo mezani kwako na kuikata mbele yako, na unawekewa kwa sahani tayari kwa kula. 
   Kusindikizia nyama hiyo, waweza kula na ugali, chipsi, wali au ndizi, na pengine waweza kuila vivyo hivyo. Labda nikudokeze bei tu, kuna ya shilingi 6,000/= na 9,000/= na kuendelea kutokana na mapenzi yako.
   Nsikuchoshe sana pata kuona mambo matamu waliyonayo.... huo ni ugali, kwa wapenda ugali
 

   Sasa kama wapenda salad au kachumbari, mpango mzima ndio huo...

   Na wale wapenda chipsi kila mara, hapa kuna zile nyembamba, tamu afu hazina kulowea mafuta, yaani kavuu

   Walijua kuna wasiopenda nyama nyekundu, hivyo mambo ya kuku wa kuchoma wakahakikisha wamejitayarisha vyema.

   Sasa hii ndo foil ya ng'ombe ambayo tayari ipo kwa sahani tayari kwa kuliwa.... wataka nini sasa??
   Hawa ndi kina Kibo Business, na uzuri nkuibie siri wanafanya kupika kwa ajili ya masherehe ya harusi, kipaimara n.k yaani pale penye mkusanyiko wa watu kwa nia ya kufurahi huku wakila nyama tamu. Wafuate uzungumze nao!!
   Kutoka Kinondoni, sie MT tunaarifu!!!

No comments:

Post a Comment