Thursday, July 19

Chachandu

  Kila mmoja wetu ana kikorombweza au niseme vikorombwezo ambavyo anapenda kusindikizia mlo wake. Kuna wanaopenda pilipili, tomato sauce, mayonnaise, chilli sauce na vinginevyo vingi tuu. Mjini Songea nilipotembelea nililetewa hii chachandu ambayo imejazwa pilipili za kutosha.
  Sio kimuonekano tuu, bali hata ladha yake ni tamu. yaani inawasha kwa sababu ya pilipili, halafu hutaki kuiacha kwasababu ya utamu. Hapo sasa!!!!


  Binafsi inategemea nakula chakula gani ndo niangalia nasindikiza na kikorombwezo gani. Tujuze wewe unapendelea kipi, na zaidi tutumie kwa picha nasi tujue, pengine tukijaribu na kukiienjoy. Karibuni sana!!

No comments:

Post a Comment