Sunday, June 3

Kiepe Mbuzi Choma.

 Hizi ni Menu za hapa na pale katika jiji la Dar es Salaam, wajua watu wengi hawapati muda wa kupika chakula chao wenyewe, hivo huwalazimu kupita katika migahawa ya vyakula na haya ni baadhi tu ya mambo yanayopatikana Dar es salaam.
  Tumekutana na sahani yenye chipsi, nyama ya mbuzi iliyochomwa, kachumbari kidogo ya kushushia mlo, na pilipili kwa waleeee wapenzi wa pilipli. Ndimu na chumvi vyasindikiza mpango mzima.....tunaamini Rafiq aliyekua anakula menyu hii alifaidi sana.

 Hizi ndo njia zetu jamani, popote tunapopita tunachukua matukio na kushare na marafiq zetu. Hii ndio MT, Karibuni Menu Time.

No comments:

Post a Comment