Wednesday, May 11

Mihogo ya Coco beach

Dar pazuri sana, katika kila aina ya chakula, kuna pahala pake ambapo wengi wetu wanapajua ndio chakula flani kinapatikana hapo, tena kwa utamu wa ajabu. Iwe kitaani au mgahawani na hata kwa nyumba ya flani.
Ukiulizia Dar wapi waweza pata crisps za mihogo na viazi fresh, ukagusia mihogo na viazi vitamu vya kukaanga, katika sehemu zitakazotajwa nina hakika Coco beach itakuwepo, almaarufu kwa Bonge.
Mchana wa leo nimepita pale, si unajua hamu tu ilinipata na kitambo sijatembele pale. kwa shilingi 1,000/=  za kitanzania niliweza pata mhogo mmoja na kiazi kimoja na chachandu yake (kachumbari si mpenzi sana hivyo nikasahau hiyo).

 
Nkashushia na maji bariiiidi, nikageuza zangu. Hii ndio sahani yangu nikiwa ndani ya gari. Karibu...

No comments:

Post a Comment