Thursday, May 23

Kifungua kinywa -Alhamisi a.k.a New Furahi dei

   Wakati tunaendelea kunako mwisho wa wiki a.k.a weekend, tunabadili muelekeo wa menu ya asubuhi a.k.a kifungua kinywa. Leo tumetoka kwenye chai, tumesogea upande wa supu.
    Supu ni mlo ambao waweza nyweka muda wowote, ukianzia na asubuhi kama kifungua kinywa, mchana katika style ya mchemsho, jioni kupasha tumbo joto kwa wale ambao hawakula chochote siku nzima, na hata kwa wale ambao hunywa kabla ya mambo yetu yaleee, na usiku pengine tukitaka kukata yalee mambo yetu, au tunapohisi hatutaki na hatuna hamu ya kula mlo mwingine, basi supu huwa suluhisho.
   Kingine supu pia hutumika sana pale tunapougua maana ni rahisi kumeza, ukiondoa uji. Hivyo wengi hupendelea kuwapikia wale wanaowauguza. Supu hutumika kama kianzio mlo kwa wale ambao wanapata ile full mlo, yaani kuanzia starter, main course na desert. Kwasasa kwenye mashughuli mengi mathalani maharusi, imekua kama ni desturi kuanza na supu au mtori, wengine wanaanza na cold desert kabla ya mlo wenyewe a.k.a ubwabwa wa harusi.
    Tujuze, huwa unakunywa supu nyakati gani? na unapendelea supu ya aina gani?? mmh je, ya kuku, samaki, ng'ombe? mbuzi au mbogamboga, hizo ni baadhi tu ya aina za supu tulizotaja, ila Rafiq tujuze ladha uipendayo.


     Hapo juu ni supu ya kuku wa kienyeji ambayo ilikutwa pande za Kigoma pajulikanapo kama land of butter and cream.
    Leo ni Alhamisi a.k.a Ijumaa mpya..... furahieni siku hii na tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuamsha salama. Siku njema tunawatakia!! 

No comments:

Post a Comment