Thursday, April 18

Kutoka mitaa ya Namanga

   Leo,tunaangalia pande za namanga, mbele kidogo baada ya kupita pale wanapopika chipsi pajulikana kwa jina la kwa Edo, hiyo sehemu ipo upande wa kulia. Wanauza chakula kitamu muno, na mara kwa mara huwa naenda nyakati za mchana kupata lunch na marafiq
   Moja ya menyu nliyokula ni wali wa nazi, pembeni kuna kisamvu ambacho kimepikwa kwa ufundi.

   Mboga ilikua ni samaki wa mchuzi na alipikwa kwa tui la nazi. Alikua mtamu munooooo
     
   Kusindikizia kulikua na maharagwe kidogo, ambayo ukiyaweka au kuchanganya na wali, basi raha tupu, huku watupia vipande vya samaki wa mchuzi wa nazi.
  
   Nilichowapendea zaidi ni kwamba, wanasikiliza wateja kwa usikivu mkubwa, wako fasta na bei zao ni zileee za kitanzania kabisa, na unatoka hapo umeshiba mno. 
   Pia wana juisi tamu mno, naongelea ya ukwaju, ubuyu, pasheni iliyochanganywa na parachichi na nyingine nyingi. kama haitoshi, pia kuna soda pamoja na maji safi baridi.
   Twaendelea kukujuza kutoka kitaani, ni sisi Menu Time team

No comments:

Post a Comment