Tuesday, July 24

Menyu toka Bagamoyo

  Baada ya purukushani za mjini Dar iiyo salama, wanafamilia waliamua kwenda nje kidogo ya mji kwenda kupunga upepo na kubadilishana mawazo. (Ni jambo jema kufanya mara upatapo mda, na inashauriwa hivyo, kwani hufanya akili kupumzika na kuweza fikiria vyema katika kupanga mipango yako ijayo)
  Kama ilivyo ada huwezi enda sehemu ikapita bila kupata menyu, na yafuatayo ndiyo yaliyojiri.
Viazi a.k.a chipsi, salad na kuku masala.


   Pia kulikua na viazi vya kuponda a.k.a mashed potatoes, na salad pamoja na kuku inayoitwa Chachandu chiken katika menyu ya Livingstone Beach Resort


Nyumbani ni nyumbani kuna walioamua kupata huyooo chachandu chiken pamoja na ugali.

   Cha ajabu kilichokutwa katika menu ya resort ya Livingstone beach ni ukosefu wa sea food na red meat, naongelea nyama ya n g'ombe, na nyinginezo. hivyo iliwapasa wanafamilia hao kuagizia kilichopo ambacho ni kuku.
   Ukipata kwenda nje ya mji, kupata kupunga hewa tujuze kupitia menutimes@gmail.com
Kutoka Bagamoyo, LJM naarifu.

No comments:

Post a Comment