Sunday, May 8

Menyu ya nyumbani - Siku ya Mama.

   Jumapili tulivu Dar Es Salaam, baada ya kukimbizana na Moshi, nipo home na leo menyu iliyopikwa kwetu ni hii. Wali wa nazi, Maharagwe yenye karanga, Samaki wa kukaanga na kachumbari (kachumbari iliyotengenezwa ni vitunguu maji, nyanya, chumvi kwa mbali na ndimu). Shukrani kwa kaka yangu kwa kukaanga samaki baada ya kuwamarinate, Bi mkubwa aliweka mkono kwenye wali na maharagwe..... lovely.
 
 
Nitumie leo Siku ya Mama wewe umekula nini, halafu tutashare na wenzetu humu ndani. Karibuni!!

No comments:

Post a Comment